20 Februari 2026 - 14:58
Source: ABNA
Kitendo cha Uadui cha Baraza la Ulaya dhidi ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC)

Baraza la Ulaya, likikamilisha vitendo vyake vya uadui dhidi ya Iran, limekiweka Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwenye kile kinachoitwa "orodha ya kigaidi."

Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA, Baraza la Ulaya likiendeleza vitendo vyake vya uadui na kufuata sera potofu za Amerika, limekiweka rasmi Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwenye ile inayoitwa "orodha ya kigaidi" ya Umoja wa Ulaya.

Kwa mujibu wa ripoti ya Al Arabiya, leo Alhamisi Baraza la Ulaya kwa misingi ya makubaliano ya kisiasa ya Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje la Umoja wa Ulaya, limetangaza kuiongeza rasmi Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwenye ile inayoitwa "orodha yake ya kigaidi."

Taasisi hii ya Ulaya inadai kuwa kwa mujibu wa uamuzi huu, fedha zote, mali za kifedha na rasilimali za kiuchumi za Jeshi la Walinzi zitafungwa (kufrizwa) katika nchi zote wanachama wa Umoja wa Ulaya.

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Ulaya hapo awali walikuwa wamekubaliana katika hatua ya kisiasa na isiyo halali kuilainisha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ambalo ni taasisi rasmi ya kijeshi ya Iran, katika orodha ya mashirika yanayoitwa "kigaidi." Hali ni kwamba wamefumba macho yao dhidi ya ukatili na mashambulizi yasiyo ya kibinadamu ya vibaraka wa CIA na Mossad dhidi ya vikosi vya usalama na raia wa kawaida wakati wa machafuko ya mwezi wa Dey (mwezi wa kalenda ya Iran) nchini Iran.

Your Comment

You are replying to: .
captcha